Thursday, December 29, 2016

TAASISI YA MO DEWIJ YATOA ZAWADI KITUO CHA TUMAI LA MAISHA

 
Taasisi ya MO Dewji Foundation imeweza kuwakumbuka watoto wanaopatiwa matibabu ya magonjwa ya kansa katika kituo cha Tumaini la Maisha kilichopo ndani ya Hospitali ya Taifa Muhimbili, Jijini Dar es Salaam. Katika kusheherekea sikukuu za mwisho wa mwaka ikiwemo kuingia mwaka mpya wa 2017, MO Dewji Foundation imeweza kutembelea watoto wa kituo hicho cha Tumaini la Maisha na kutoa zawadi kwa watoto hao ili kuwasaidia katika kipindi wawapo kituoni hapo

Wednesday, December 28, 2016

NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI AFANYA ZAIARA MANYONI, MKOANI SINGIDA


jofo-5
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Selemani Jafo akiangalia kitanda ambacho inatumiwa na akina mama wajawazito wakati wa kujifungua katika Hospitali ya wilaya ya Itigi mkoani singida wakati alipofanya ziara ya kushtukiza. Kulia kwake ni Dkt. Mary Rume Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya Itigi na anayefuatia ni Mkuu wa wilaya Manyoni Geoffrey Mwambe.

BODI YA MIKOPO IMESEMA ITAYAANIKA MAJINA NA PICHA ZA WADAIWA SUGU HADHARANI.

BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imesema kuanzia mwanzoni mwa Januari mwakani, itaanza kuchapisha majina na picha za wadaiwa sugu kwenye vyombo vya habari waliohitimu katika vyuo mbalimbali vya elimu ya juu kuanzia wale wa miaka 10 iliyopita.

AFUMWA AKISHI NA MWANAFUNZI NYUMBANI KWAKE

WANANCHI katika kijiji na kata ya Guta, wilaya ya Bunda mkoani Mara, wamelalamikia vitendo vinavyofanywa na baadhi ya walimu katika kata hiyo, kwa kufanya ngono na wanafunzi na kuishi nao kinyumba kama wake zao.

Hatua hiyo ya kulaani inatokana na hivi karibuni kumkamata mwalimu wa shule ye Msingi Guta, akiishi na mwanafunzi wa shule hiyo kinyumba kama mkewe.

MAGAZETI YA LEO DE- 29- 2016


YANGA YAIPA PRESHA SIMBA, BAADA YA KUSHINDA 4-0.

 Golikipa wa Ndanda FC, Jeremiah Kisubi akiokoa moja ya hatari langoni mwake wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara dhidi ya Yanga. Yanga imeshinda 4-0. (Picha na Francis Dande).
Wachezaji wa Yanga wakipongezana baada ya Amis Tambwe kuipatia timu yake bao.

MAAMUZI YA RUFAA YA LEMA KUJULIKANA JANUARI 4, 2017


Na Vero Ignatus 
Mahakama kuu kanda ya Arusha imesikiliza maombi ya rufaa yayaliyowasilishwa na upande wa jamhuri na ule wa mshtakiwa Godbless Lema ambapo pande zote mbili wamekubaliana kusikilizwa rufaa ya upande wa jamhuri ambapo upande wa serikali wameiomba mahakama kuwasilisha kwa hati ya maandishi hapo kesho tarehe 30 Disemba 2016 

Polisi Morogoro wawashikilia watuhumiwa 12 Watuhuniwa waliomchoma Mkuki Pius

Jeshi la Polisi mkoa wa morogoro linawashikilia watu kumi na wawili kwa tuhuma za kumjeruhi na kumchoma mdomomi mkuki uliotokezea shingoni Augustino Pius mkazi wa kijiji cha Dodoma Isanga wilayani kilosa ambapo saba kati yao tayari wamekifishwa mahakamani.

Akiongea na waandishi wa habari kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa morogoro Ulrich Matei amesema kuwa wafugaji jamii ya kimasai wilayani kilosa mkoani morogoro waliwashambulia wakulima kwa silaha za jadi na kuwajeruhi watu sita mara baada ya kukamatwa kwa mifugo ilioyokuwa inaharibu mazao shambani.

Tuesday, December 27, 2016

MAKUBWA YAIBUKA KWA MTOTO ALIYEFIA HOTELINI HUKU AKIONGELEA SIKU YA CHRIS-MASS.

SAKATA la mtoto wa miaka 12 aliyekufa wakati akiogelea katika bwawa la hoteli ya kitalii ya Mount Meru mjini hapa, limechukua sura mpya baada ya kugundulika kuwa bwawa hilo lilijaa damu baada ya kifo chake.

Kamanda wa Polisi mkoani Arusha, Charles Mkumbo amethibitisha madai ya mashahidi waliokuwa eneo la tukio, waliodai kuwa bwawa la kuogelea la hoteli hiyo liligeuka kuwa dimbi la damu wakati mwili wa mtoto huyo ukiopolewa kutoka bwawa hilo, siku ya Krismasi.

FAIDA ZA TUNDA, CHUNGWA KATIKA MWILI WA BINADAMU.

KUMEKUWA na sababu mbalimbali zinazofanya watu kutokuwa na ngozi zisizokubalika.Mbali na hali ya hewa pia matumizi ya pombe na sigara hata matumizi ya cream kali ambazo zimekuwa zikitumiwa na watu bila kujua madhara yake kumechangia kwa kiasi kikubwa tatizo hilo.

MTU MMOJA AFARIKI DUNIA NA NYOKA WAKE.

DUNIANI kuna mambo, ndivyo unaweza kusema kutokana na mkazi wa Mtaa wa Mateka, Manispaa ya Songea, Denis Komba (26) kufa baada ya nyoka wake aliyekuwa amembeba kwenye mfuko wa jaketi kuuawa na wananchi.

Komba alifariki dunia katika hospitali ya Rufaa Songea mkoa wa Ruvuma (Homso) ambako alilazwa baada ya watu wenye hasira kumuua kwa mawe na fimbo nyoka wake huyo.

WALIOFAULU USAILI WA KAZI SERIKALINI WATAKIWA KUOMBA AJIRA UPYA.

Waliofanya usahili serikalini, wakafaulu lakini kabla ya kupangiwa vituo vya kazi ajira zikasitishwa; watakiwa kuomba ajira upya.Taarifa ya Sekretarieti ya Utumishi wa Umma imesema kuwa huo ni utaratibu wa kawaida wa sekretarieti hiyo

MAGAZETI YA LEO DEC-28- 2016


img_20161228_055829
img_20161228_055842
img_20161228_055722

TUME YA MIPANGO YATEMBELEA UJENZI WA JENGO LA TERMINAL III, UWANJA WA NDEGE WA JULIUS NYERERE DAR ES SALAAM.

 Meneja mradi wa ujenzi wa kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Mhandisi Mwanaidi Mkwizu (aliyevaa suti) akitoa melezo kwa Timu ya ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Tume ya Mipango.

MOTO WATEKETEZA NYUMBA 50 WAMILIKI WAKE WAKILA KRISMASI

MOTO mkubwa umezuka na kuteketeza nyumba zaidi ya 50 katika kisiwa cha Kasalazi kilichopo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa mkoani Mwanza.

Tukio hilo lilitokea juzi saa 3:00 usiku, linadaiwa kuwa ni la nne kutokea kisiwani humo katika miaka ya karibuni.

Imeelezwa kuwa moto huo ulizuka na kuteketeza nyumba hizo huku wamiliki wake wakiwa kwenye shamra shamra za Krismasi.

Nyumba zilizoteketea kwa moto ni zile zilizojengwa kwa kutumia mabanzi ya miti, mbao na kuezekwa kwa maturubai, nyasi na baadhi kwa bati.Chanzo cha moto huo bado hakijafahamika.

WALIOFAULU NI LAZIMA WAENDE SEKONDARI .

*Asema atafuatilia ajue kwa nini kuna tozo kwenye maghala ya Serikali

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali haitavumilia kuona mamia ya vijana waliofaulu mitihani ya darasa la saba na kuchaguliwa kuingia kidato cha kwanza wanabaki nyumbani eti kwa kuwa hakuna madarasa ya kutosha.

“Serikali haitaridhika kuona vijana waliofaulu vizuri wanashindwa kwenda kidato cha kwanza. Halmashauri zilijua tangu mapema ni wanafunzi wanaenda shule za msingi kwa hiyo inataka kuona wote waliofaulu wanakwenda sekondari kwa asilimia 100,” amesema.

Ametoa kauli hiyo leo mchana wakati akizungumza na viongozi na watendaji wa mkoa wa Lndi mara baada ya kupokea taarifa ya mkoa huo kwenye Ikulu ndogo wilayani Nachingwea. Waziri Mkuu amewasili wilayani Nachingwea akiwa njiani kuelekea Ruangwa kwa mapunziko ya mwisho wa mwaka.

Amesema Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kutoa elimu ya bure kwa kila mtoto sasa iweje watoto wengine wanafaulu na wanashindwa kujiunga na elimu ya sekondari. “Tumesema elimu ni bure hakuna sababu ya kufanya wengine wasiende shule wakati azma ya Serikali ni kutoa elimu ya bure. Hakikisheni wote wanaingia katika chaguo la kwanza,” amesema.

Monday, December 26, 2016

JE WAJUA UMUHIMU WA PAPAI?

ASILI ya mpapai ni Amerika ya Kati, ambapo kuanzia matunda, majani na utomvu wa mmea huu hutumiwa kama dawa maeneo mbalimbali duniani. Vile vile, matunda na utomvu wake yamekuwa yakitumika kutengeneza pombe na mvinyo katika baadhi ya nchi, huku wengine wakitumia mpapai kama dawa kwa mifugo na binadamu.

SERIKALI YAENDELEA KUTO DAWA ZIZAZO TIBU SUMU YA NYOKA

SERIKALI imesema itaendelea kutoa dawa zinazotibu sumu ya nyoka ili kupambana na tatizo hilo nchini. Kauli hiyo ya serikali ilitolewa Dar es Salaam jana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu.


“Kama tunavyofahamu nchi yetu ina aina mbalimbali za nyoka ambao pindi wakimuuma mtu huleta madhara mbalimbali ya kiafya. Aidha tunafahamu kwamba tatizo hili lipo zaidi katika maeneo ya vijijini ambako uwezo wa wananchi kumudu gharama za matibabu ni mdogo.”

VYAKULA HATARI KWA WANAUME,USIVITUMIE MARA KWA MARA.




Spearmint:
Hutumiwa zaidi kama kiambata kwenye chewing gums, candies, na breath freshener au kwenye majani ya chai (herbal tea). Spearmint pia in akiwango kikubwa cha estrogen

 
 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhvFso2GGfQQa7QqGqGpXoDZRy93Ca2wzROl1yqiSqihb85v3F6PTHPh8LcEthbfwogD_xeSBD6_QGMD6THvP0sBjV7ZtyaVoJtwbcdpyVCE5JvM7dwwG1X0OBWGCCt3aoXujeF-ho8Vb0/s400/1.jpg



Mbegu za Flax (Flax seeds):  

Wanaume wanapaswa kufahamu aina ya vyakula ambavyo si rafiki kwao katika kuongeza kiwango cha homoni ya kiume iitwayo testosterone inayochochea sifa ya mwanaume yaani kuwa na nguvu za kiume. Baadhi ya vyakula visivyofaa kuliwa na mwanaume aliyetaka kuwa na nguvu za kiume ni vile vyenye asili ya homoni ya kike iitwayo estrogen. Hivyo sio kila vyakula vinafaa kwa mwanaume eti ilimradi tu vyakula hivyo vinasaidia kujenga mwili au kujaza tumbo wakati mtu akiwa na njaa.

MAGAZETI YA LEO DEC-27-2016



MWANAFUZI AMEFARIKI DUNIA WAKATI AKIOGELEA SIKU YA CHRS-MASS

MWANAFUNZI wa darasa la tano wa Shule ya Msingi Sekei iliyopo jijini Arusha, Cliff Laiza (12) amekufa wakati akiogelea kwenye bwawa lenye kina kirefu katika Hoteli ya Kitalii ya Mount Meru iliyopo jijini hapa katika sherehe ya Krismasi.

Tukio hilo ni la juzi majira ya saa 12 jioni wakati Cliff na watoto wengine, walipokuwa wakiogelea katika hoteli hiyo, ikiwa ni sehemu ya kusherehekea Krismasi.

WACHEZAJI WA YANGA MAMBO SAFI SASA HIVI ,WAPEWA MAMILIONI YAO.

Hatimaye kimeleeweka, hivi ndivyo utakavyoweza kutamka baada ya uongozi wa Yanga kuwalipa wachezaji wake mshahara na posho zao za mechi za Ligi Kuu Bara walizocheza.

Hiyo imekuja siku chache baada ya wachezaji hao kugomea mazoezi ya timu hiyo kwa siku mbili mfululizo, wakidai mshahara wa Novemba, mwaka huu.

Kwa mujibu wa chanzo kutoka kwenye benchi la ufundi la timu hiyo, wachezaji hao walilipwa mshahara na posho hizo juzi Ijumaa.

TAARIFA ZA KUSIKITISHA KUTOKA MANZESE DAR-ES- SALAAM

 OFISI YA MBUNGE Jimbo La Mikumi inalaani sana kitendo cha kinyama kilichofanywa na Ndugu zetu wa jamii ya wafugaji kwa kujichukulia sheria mkononi na kumjeruhi vibaya Ndugu Augustino Mtitu mkulima wa kitongoji cha Upangwani, Kijiji cha Dodoma Isanga, Kata Ya Masanze Jimbo la Mikumi ambapo leo tarehe 25 Desemba majira ya Mchana amechomwa mkuki mdomoni na kutokezea nyuma ya shingo yake, ambapo alipelekwa hospitali ya wilayani Kilosa na baadae amekimbizwa hospitali ya mkoa Morogoro  ili kufanyiwa operesheni ya kuondoa mkuki huo na kwa matibabu zaidi.

MKUU WA MKOA WA ARUSHA AZUNGUMZIA SAKATA LA MWANDISHI WA HABARI.

Sakata la mwandishi wa habari wa ITV Halfan Lihundi kukamatwa na kuwekwa mahabusu kwa saa 24 kwa amri ya mkuu wa wilaya ya Arumeru baada ya kuandika habari ambayo haikumfurahisha mkuu huyo, limechukua sura mpya baada ya mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo kuingilia kati na kusema waandishi wa habari wanao uhuru wa kuandika habari mahali popote katika mkoa huo ili mradi wazingatie weledi katika taaluma.

TAARIFA JUU YA UVUMI KUHUSU NOTI YA MIA TANO.

Benki kuu ya Tanzania inapenda kuwafahamisha wananchi wote kuwa,habari inayoenea katika mitandao mbalimbali ya kijamii kwamba noti ya shilingi mia tano  haitatumika tena kuanzia Desemba 31, 92016; sio taarifa ya kweli na ni uvumi unaopaswa kupuuzwa.
Ukweli ni kwamba noti ya shilingi 500 itaendelea kuwepo katika mzunguko sambamba na ile sarafu ya shilingi 500 hadi pale noti hiyo itakapotoweka mikononi mwa wananchi. Tafadhali mpuuze taarifa hizo sio za ukweli.

Marcian Kobello.
Mkurugenzi wa Huduma za kibenki- BoT .