Saturday, May 3, 2014

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AZINDUA RASMI SHEREHE ZA MBIO ZA MWENGE WA UHURU MKOANI KAGERA


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,

WACHEZAJI WA ENGLAND WATISHA KWA KUVAA SUTI ZA BEI KALI, KWA AJILI YA KOMBE LA DUNIA MWAKA HUU,

Dressed to impress: England players (from left to right) Andros Townsend, Adam Lallana, Jermain Defoe, Leighton Baines, Steven Gerrard, Ashley Cole, Frank Lampard, Chris Smalling, Michael Carrick, Gary Cahill, John Ruddy and Rickie Lambert show off the Three Lions' Marks and Spencer suits for this summer's World Cup

WAANDISHI WA HABARI UNGANENI.

DSC_0017
Baadhi ya waandishi wa habari na wadau kutoka asasi mbalimbali nchini wakifanya usajili kwenye kongamano la siku moja lilioandiliwa kuadhimisha Uhuru wa vyombo vya Habari Duniani 2014 lililofanyika jijini Arusha.(Picha na Zainul Mzige).

Na Waandishi Wetu, Arusha
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Absalom Kibanda ametoa wito kwa waandishi wa habari nchini kuyapa uzito matukio yanayowatokea waandishi wa habari na kuyapigia kelele kwa nguvu zote ili kuyakomesha.
Kibanda aliyasema hayo jana mjini Arusha katika kongamano lililoandaliwa kama sehemu ya maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani na kuongeza kwamba wakati umefika kwa waandishi wa habari kuondoa tofauti zao na kuungana pamoja kuongeza nguvu waliyonayo kukabiliana na ukatili unaoendelea dhidi ya waandishi wa habari katika miaka ya hivi karibuni.
“Baadhi ya wahariri huwa hawayaandiki madhila yanayowasibu waandishi wa habari na kuyapa uzito unaostahili aidha kwa huyapuuzia au kudharau kwa kuwa hayawahusu moja kwa moja,” alisema Kibanda.
Aliongeza kwa kusema kuwa vyombo vya habari mara nyingi vimekuwa vikinyooshewa vidole na kulaumiwa kwa kutokufanya kazi kwa uadilifu jambo ambalo linatafsiriwa kuwa ni la uonevu, vinatumiwa vibaya na hakuna anayesimama kuvitetea kutokana na mchango wake mkubwa katika jamii.
DSC_0053
Afisa Mipango Kitengo cha Mawasiliano, Habari na Tehama UNESCO, Bw. Al Amin Yusuph, akiwasilisha mada kuhusu mchango wa uhuru wa vyombo vya habari katika utawala bora, kukuza uwezo na kupunguza umaskini kongamano la waandishi wa habari lilioandaliwa kama sehemu ya maadhimisho ya siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yanayofanyika jijini Arusha.

“Kwa sasa tasnia hii iko kwenye wakati mgumu sana kwani hata marais wa nchi mbalimbali mfano Uganda, Kenya hata Marekani wanakinzana na vyombo vya habari kwa madai kuwa kauli zao zinapotoshwa, laikini ukweli ni kwamba ni vyema kauli hizo za viongozi zikachunguzwa kwa undani zaidi ili kuelewa iwapo zina uwajibikaji ndani yake,” alisema Kibanda.
Kibanda aliongeza kuwa wakati umefika sasa kwa waandishi kutambua kuwa kuna ajenda za siri zilizojificha dhidi ya uteswaji wa waandhishi wa habari hivyo yasidharauliwe, yafanyiwe kazi kwa kina ili kuelewa kiini cha tatizo kwa kupata ufumbuzi.

Kwa upande wake mwandishi mkongwe na aliyetunukiwa tuzo ya maisha mwaka 2012 na Baraza la Habari Hamza Kasongo alisema vyombo vya habari vina nguvu kubwa katika kushawishi hivyo vitumie nguvu hiyo kama muhimili wa nne wa nchi katika kuzikabili changamoto zilizopo.
“Kuwe na mtandao unaoeleweka wa mawasaliano kati ya waandishi wa habari nchini ili kuhakikisha kuwa matatizo yaliyopo yanatatuliwa bila woga na kwa ujasiri kwa lengo la kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa,” alisema Kasongo.
DSC_0060
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Kitivo cha Sheria , Bw. James Jesse, akitoa mada kuhusu umuhimu wa sheria katika kulinda haki ya uhuru wa kujieleza kwa kila mtu wakati wa kongamano la waandishi wa habari lilioandaliwa kama sehemu ya maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani yanayofikia kilele leo jijini Arusha.

Mwanahabari mwingine mkongwe Dokta Samwilu Mwaffisi aliyetoa mada ya Maadili ya Uandishi wa Habari alisema kuwa kuna haja ya waandishi kuzingatia uhuru wa habari walionao kwa kuzingatia maadili yanayowaongoza ili kuboresha heshima waliyonayo katika jamii kwa kuandika ukweli na uhakika, bila upendeleo, kutoa fursa ya kujitetea na kukubali kuomba radhi pale unapokosea.
“Kuandika habari zenye kuzingatia maadili kunapunguza manung’uniko, mashauri na kuongeza heshima ya chombo cha habari na mwanahabari mwenyewe,”
Akizungumzia suala la ufanisi, Rais wa Vilabu vya Waandishi wa Habari, Kenneth Simbaya, aliwaasa waandishi wa habari kusimamia ukweli katika kazi zao na kuacha kufanya kazi kwa mazoea jambo ambalo litakawaweka huru zaidi katika utekelezaji wa shughuli zao za uandishi wa habari.
Maadhimisho hayo yaliyoandaliwa na umoja wa asasi mbalimbali chini ya uenyekiti wa MISA TANZANIA unafikia kilele chake tarehe 3 Mei kwa kuzindua majarida mbalimbali, matamko kutoka asasi mbalimbali na kuhitimishwa kwa tafrija ya chakula cha jioni chini ya mgeni rasmi Jaji Mstaafu Mheshimiwa Mark Bomani.
DSC_0341
Mwanahabari Mkongwe kutoka Chuo Kikuu Huria, Dokta Samwilu Mwaffisi (kulia) akiwasilisha mada ya Maadili ya Uandishi wa Habari kwenye kongamano la siku moja lilioandiliwa kuadhimisha Uhuru wa vyombo vya Habari Duniani 2014 lililofanyika jijini Arusha. Kushoto ni Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Iringa, Bw. Simon Berege.
DSC_0311
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Absalom Kibanda, akitoa maoni yake wakati wa kongamano la siku moja lilioandiliwa kuadhimisha Uhuru wa vyombo vya Habari Duniani 2014 lililofanyika jijini Arusha.
DSC_0079
Pichani juu na chini ni baadhi ya waandishi wa habari wakongwe, mabalozi na wanahabari washiriki katika kongamano la siku moja lilioandiliwa kuadhimisha Uhuru wa vyombo vya Habari Duniani 2014 lililofanyika jijini Arusha.
DSC_0028
DSC_0283
DSC_0371
Mwandishi wa Habari Chokonozi, Bw. Fredrick Katulanda, akielezea madhila mbalimbali yaliyomsibu katika utekelezaji wake wa kuandika habari za uchambuzi.
DSC_0119
Mwanahabari Mkongwe Bi. Leila Sheikh akichangia mada ya Mchango wa Uhuru Wa Vyombo Vya Habari Katika Utawala Bora, Kukuza Uwezo Na Kupunguza Umaskini wakati wa kongamano la siku moja lilioandiliwa kuadhimisha Uhuru wa vyombo vya Habari Duniani 2014 lililofanyika jijini Arusha.
DSC_0348
Mmiliki wa Gazeti tando la Mjengwa na Kituo cha Redio Kwanza Jamii, Bw. Maggid Mjengwa akielezea jinsi Intaneti inavyoweza kuunganisha mtandao wa Redio.
DSC_0339
Makamu Mwenyekiti wa Mtandao wa Vyombo vya Habari Jamii Tanzania (COMNETA) na Mkurugenzi wa kituo cha mawasiliano Sengerema, Bw. Felician Ncheye akichangia mada.
DSC_0386
Mkufunzi wa Redio Jamii kutoka UNESCO, Mama Rose Haji Mwalimu, (kushoto) akiwa na baadhi ya washiriki wa Kongamamo hilo.
DSC_0310
Rais wa Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa habari Tanzania (UTPC) Bw. Kenneth Simbaya, akishiriki kwenye kongamano la siku moja lilioandiliwa kuadhimisha Uhuru wa vyombo vya Habari Duniani 2014 lililofanyika jijini Arusha.
DSC_0281
Picha juu na chini Baadhi ya washiriki wakichangia maoni yao kwenye kongamano la siku moja lilioandiliwa kuadhimisha Uhuru wa vyombo vya Habari Duniani 2014 lililofanyika jijini Arusha.
DSC_0322
DSC_0214
Kongamano la siku moja lilioandiliwa kuadhimisha Uhuru wa vyombo vya Habari Duniani 2014 likiendelea.
DSC_0164
Mwanakamati wa maandilizi ya maadhimisho ya Kongamano la Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014, Usia Nkhoma Ledama wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Absalom Kibanda nje ya ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa AICC jijini Arusha

KINANA LEO KUHUTUBIA PEMBA. Soma zaidi

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (ZNZ) Vuai Ali Vuai mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege Pemba, Katibu Mkuu anatarajiwa kufanya mkutano wa hadhara Pemba

Friday, May 2, 2014

NJIA SABA (7) ZA HUAKIKA ZA KUPATA AJIRA KWA URAHISI HIZI HAPOA.


Kupata nafasi za ajira imekuwa ngumu siku hadi siku, hususani ukitilia maanani kuwa wahitimu wanazidi kuwa wengi na hali ngumu ya uchumi inafanya waajiri kushindwa kuongeza nafasi mpya za kazi. Hauna haja ya kukata tamaa ya kupata kazi ile unayoitarajia hata kama kuna ukiritimba mwingi katika soko la ajira kama vile watu kupeana kazi kwa kujuana, nafasi za kazi kutotangazwa  au kazi haipatikani mpaka rushwa itembee. Makala hii inaenda kujadili mambo ya msingi kwa yeyote anayetafuta kazi, uwe kwa sasa umeajiriwa unatafuta kazi mbadala au uwe hauna ajira unatafuta ajira, bila shaka mambo tunayojadili hapa yatakusaidia.

Mahakamani kwa kumtusi Rais Kenya


Mtuhumiwa Samuel Aboko
Mwanasiasa mmoja mwakilishi wa Wodi, nchini Kenya ameshitakiwa kwa madai ya kumtusi Rais Uhuru Kenyatta katika mkutano wa kisiasa uliofanyika katika jimbo la Kisii Magharibi mwa Kenya
Kwa mujibu wa mtandao wa Daily Nation, mwakilishi huyo wa wodi ya Kiogoro Samuel Aboko Onkwani, anadaiwa kusema maneno haya:
''Washirika wa karibu wa Rais Uhuru Kenyatta wanapaswa kumshauri awache kuvuta Bhangi.’’

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI YATANGAZA NAFASI ZA MAFUNZO YA UALIMU KWA MWAKA WA MASOMO 2014/15,WENYE DIVISION FOUR YA 32 HADI 34 RUKSA KUAPPLY.

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi inatangaza nafazi za Mafunzo ya Ualimu ngazi ya Stashahada na Cheti kwa Mwaka wa Masomo 2014/2015.
Kuzidownload bofya link hizo hapo chini, ya kwanza ngazi ya cheti (Certificate Grade A) na ya pili ni stashahada (Diploma).

JE WAJUA MIPAKA YA HAUSI GELI NDANI YA NYUMBA. Hii hapa

Ni matumaini yangu kwamba umzima na unaendelea vyema na shughuli zako za kila siku kama kawaida. Mimi niko poa, namshukuru Mungu kwa kunifanya kuwa miongoni mwa wale wanaoendelea kupumua hadi leo.

Mpenzi msomaji wangu, wiki iliyopita utakumbuka nilianza kuzungumzia mada hii. Leo nitaenda moja kwa moja kwenye ile mipaka ya hausigeli ndani ya nyumba nikiamini mwisho wa siku wanandoa watajifunza kitu kitakachoziboresha ndoa zao.

Kikwete:Katiba siku 60 tu

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia katika kilele cha Siku ya Wafanyakazi Duniani (MEI MOSI) leo Mei 1, 2014 katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
PICHA NA IKULU
Rais Jakaya Kikwete, amesema iwapo siku 60 za nyongeza zitakwisha bila wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba kufikia maridhiano na kupata Katiba mpya, hakutakuwa na nyongeza nyingine ya muda.

Rais Kikwete aliyasema hayo jana wakati akihutubia maelfu ya wafanyakazi katika sikuku ya Mei Mosi ambazo Kitaifa zilifanyika kwenye Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam.

Thursday, May 1, 2014

MKUTANO WA 12 WA SIKU MOJA WA VIONGOZI WAKUU WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI JIJINI ARUSHA

Wakuu wa Mataifa ya Jumuiya ya Afrika Mashariki wakizindua kitabu rasmi cha Muongozo wa Majaji wa Jumuiya hiyo kwenye Mkutano wa 12 wa siku moja wa Jumuiya hiyo uliofanyika ukumbi wa Kimataifa wa Arusha { AICC }.

ENEO LA AJALI YA SUMRY SINGINDA, NA LILIVYO UWA ASKARI WA BARABARANI.



Majeneza yenye miili ya askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani waliofariki dunia baada ya kugongwa na basi wakati wakipima ajali katika kijiji cha Utaho wilani Ikungi mkoa wa Singida kabala ya kuagwa na kusafirishwa kwenda makwao. Picha na Gasper Andrew

WAWINDAJI HALALI NDIYO WANAO VUNA TEMBO. Soma Zaidi.


Uchunguzi huo ulibaini kuwa vinasaba vya pembe hizo vilifanana, hivyo kujenga dhana kwamba baadhi ya watu wamekuwa wakiwinda katika hifadhi hiyo mara kwa mara katika utaratibu maalumu unaotambuliwa na Serikali.PICHA|MAKTABA

SHEREH YA MEI MOSI MWANYA YAFANYIKA, WAFANYAKAZI WAOMBA KODI IPUNGUZWE, MSHAHARA UWONGEZWE.

 Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa wakipita ya mgeni wa heshima Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Eng.Evarist Welle Ndikilo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi mkoa wa Mwanza ,matembezi hayo yalihitimishwa kwenye uwanja wa CCM Kirumba.

GARI LA FREEMAN MBOWE LILILO KAMATWA KENYA. Soma zaidi Hapa..

Screen Shot 2014-05-01 at 1.50.04 PMNi magazeti kadhaa ya leo Tanzania ambayo yameripoti kuhusu kukamatwa kwa gari la Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe huko Mombasa Kenya.

NI ATLETICO NA REAL MADRID KATIKA FAINALI YA UEFA.

Ni Atletico Madrid na Real Madrid katika fainali
Matumaini ya Chelsea ya Uingereza kufuzu katika fainali yao ya tatu ya kombe la mabingwa barani Ulaya katika kipindi cha miaka sita iligonga mwamba uwanjani Stamford Bridge baada ya Atletico Madrid ya Uhispania kutoka nyuma bao moja kwa nunge katika kipindi cha kwanza na kuilaza the blues mabao matatu kwa moja katika mechi ya mkondo wa pili.

MAHAKAMA MORO YAMSHUKURU SHEIKH PONDA. soma zaidi hapa.










 
WAFANYAKAZI wa Mahakama ya Hakimu mkazi mkoa wa Morogoro wamesema ujio wa kesi ya
Katibu wa Taasisi na Jumuiya za Kiislamu nchi Sheikh Ponda Issa Ponda mahakamani hapo umesaidia kubadilisha mandhar ya Mahakama hiyo.