Sakata
la mwandishi wa habari wa ITV Halfan Lihundi kukamatwa na kuwekwa
mahabusu kwa saa 24 kwa amri ya mkuu wa wilaya ya Arumeru baada ya
kuandika habari ambayo haikumfurahisha mkuu huyo, limechukua sura mpya
baada ya mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo kuingilia kati na kusema
waandishi wa habari wanao uhuru wa kuandika habari mahali popote katika
mkoa huo ili mradi wazingatie weledi katika taaluma.
Gambo
ambaye wakati sakata hilo linatokea alikuwa safarini analazimika
kukutana na wanahabari wote wa jiji la Arusha baada ya tukio hilo
lililogoga vichwa vya waandishi mkoa wa huo na kusababisha kusimamisha
shughuli zao ikiwemo kuweka kalamu chini kumnusuru mwenzao lakini pia
wadau mbalimbali tasnia ya habari kukerwa na kitendo hicho.
Gambo
amesema anatambua umuhimu wa kazi za waandishi wa habari na kuongeza
kuwa kabla ya kiongozi huyo hajafanya maamuzi hayo pamoja na mamlaka
aliyonayo busara ilitakiwa itumike.
No comments:
Post a Comment