Akionyesha ishara ya kuombea wenye maradhi ya saikolojia.
Sunday, June 1, 2014
SHEKH SHARIF, AKIFANYA MAMBO.
Akionyesha ishara ya kuombea wenye maradhi ya saikolojia.
AMFUNGA MAMA YAKE MZAZI MIAKA 2
“Siwezi
kukupa comment (maoni) kwa sababu lipo kwenye uchunguzi maana suala
hili nimewapatia polisi walifanyie uchunguzi, kwa hiyo wakishamaliza
utaratibu wa kuchunguza wakapata ukweli wa hili jambo watanipa taarifa
hivyo nitakuwa kwenye position (nafasi) ya kusema kwa hiyo nategemea
kuletewa taarifa kamili kwa maandishi,” anasema Kilasi.
Hata
hivyo Evaristo Ng’ande, kijana anayedaiwa kumfungia ndani mama yake
huyo wa kambo alipotafutwa kutolea ufafanuzi suala hilo alisema hawezi
kuzungumza chochote kwa kuwa ameshatoa maelezo polisi hivyo anasubiri
polisi wakamilishe uchunguzi wao wampeleke mahakamani.
“Yaani
habari za mgonjwa huyo mimi siwezi kusema chochote maana maelezo yangu
nimeshatoa polisi na kesi yangu iko polisi, kwa hiyo nasubiri
wakamilishe uchunguzi wao nipelekwe mahakamani,” alisema Ng’ande kwa
kifupi.
Ban Ki Moon ampongeza JK katika kupugania Afya ya Mama – Mtoto
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Katibu
Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon.(Picha na Maktaba).
Katibu Mkuu
wa Umoja wa Mataifa amesifu jitihada za Rais Jakaya Mrisho Kikwete na
mchango wake mkubwa katika kupigania Afya ya Mama na Mtoto.
Bw. Ban Ki
Moon ametoa pongezi hizo tarehe 30 Mei,2014 wakati alipokuwa
akizungumzia juhudi za kumuokoa Mama na Mtoto baada ya Mwaka 2015,
mwishoni mwa mkutano wa siku 3 kuhusu Afya ya Mama na Mtoto kama
ilivoainishwa katika Malengo ya Milenia .
SIASA, KITAIFA, KIMATAIFA, MICHEZO,
HOME,
KIMATAIFA,
KITAIFA,
MICHEZO.,
SIASA. ULIMWENGU. KITAIFA
VIJANA WAASWA KUACHA KUJIINGIZA KATIKA MAPENZI KATIKA UMRI MDOGO.
Afisa Msaidizi wa Vijana kituo cha
UMATI tawi la Dar es Salaam Bi. Upendo Daud akiwaeleza vijana kuhusu
mada kuu ya Tamasha ambayo ni “Athari za ndoa za utotoni” wakati wa
ufunguzi wa tamasha la mwezi katika kituo hicho.
SIASA, KITAIFA, KIMATAIFA, MICHEZO,
HOME,
KITAIFA,
MICHEZO.,
SIASA. ULIMWENGU. KITAIFA
WAISILAMU ZAIDI YA 300, WACHANGIA DAMU KATIKA HOSPITALI YA RUFAA MKOA WA IRINGA.
SIASA, KITAIFA, KIMATAIFA, MICHEZO,
HOME,
KITAIFA,
SIASA,
SIASA. ULIMWENGU. KITAIFA
PETER MUTHALIKA, AAPISHWA KUWA RAIS MPYA WA MALAWI.
Peter Muthirika anayeongoza chama cha DPP ndiye rais mteule nchini Malawi
Hatimaye Malawi imepata Rais mpya baada ya mivutano ya kisheria kwa wiki nzima.Mwandishi wa BBC Baruan Muhuza amesema kutoka mjini Blantyre kuwa Profesa Peter Mutharika ameshinda uchaguzi huo kwa kupata asilimia 36.4 ya kura zote akifuatiwa na Dr Lazarus Chakwera mwenye asilimia 27.8 huku Rais anayemaliza muda wake Dr Joyce Banda akishika nafasi ya tatu kwa asilimia 20.2 na Atupele Muluzi amekuwa wa nne na asilimia 13.7
SIASA, KITAIFA, KIMATAIFA, MICHEZO,
HOME,
KIMATAIFA,
KIMATAIFA MICHEZO,
MICHEZO.,
SIASA,
SIASA. ULIMWENGU. KITAIFA
ZAIDI YA ASILIMIA 20 YA WALIMU, WANAWANYWESHA MATONGO POLI WANAFUNZI,
Dar es Salaam.
Wakati Serikali ikiahidi kuboresha elimu nchini kwa kuhakikisha
inaajiri walimu wa kutosha, imebainika kuwa asilimia 25 ya walimu
huwafundisha wanafunzi mambo yasiyo ya msingi.
Ripoti ya
Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (Unesco),
iliyozinduliwa Dar es Salaam hivi karibuni, imebainisha kuwa wakati
wananchi wakilalamika kuwa elimu inayotolewa haimsaidii mwanafunzi
kupata ajira nzuri, wanafunzi hawajifunzi mambo ya msingi
yatakayowasaidia kupambana na changamoto za maisha.(FS)
SIASA, KITAIFA, KIMATAIFA, MICHEZO,
HOME,
KITAIFA,
MICHEZO,
SIASA,
SIASA. ULIMWENGU. KITAIFA
Subscribe to:
Posts (Atom)