Monday, August 18, 2014

JUDGE LEWIS MAKAME AFARIKI DUNIA.

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Lewis Makame amefariki Dunia katika Hospital ya AMI Trauma Center, Masaki - Dar
- Alikuwa amelazwa hapo tangu mwezi Julai, 2014 (mwezi uliopita)

PALE AMBAPO MBWA ANAKUA NA THAMANI KULIKO MTOTO, KATIKA BARA YA ULAYA.


THAMANI YA MBWA MBELE YA MTOTO WA BINADAMU HUKO DUNIA YA KWANZA ILIVYO, SIO JAMBO LA KUIGA HILO HATA PUNJE

MAULIDI ITENGE AONDOKA RADIO ONE

Maulid Kitenge.
MTANGAZAJI wa michezo wa Radio One Stereo, Maulid Kitenge kupitia akaunti yake ya Twitter hivi punde ametangaza kuondoka rasmi katika radio hiyo baada ya kuitumikia kwa miaka 14. Kupitia Twitter, Kitenge ameandika hivi:

MTEMVU AZIDI KUFANYA MAMBO MAKUBWA TEMEKE


 Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu ameendelea kumwaga misaada kwa wadau na makundi mbalimbali ya wananchi katika jimbo lake, Pichani, Mtemvu akizungumza kabla ya kuanza kugawa zawadi hizo kwa ambao hawakuzipata wakati wa Mfungo uliopita wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, zaidi ya wananchi 900 walipata zawadi hizo alizogawa jana kwenye viwanja vya Manispaa ya Temeke, Dar es Salaam.
 Mtemvu akionyesha chupa ya chai ambayo ni miongoni mwa seti za vifaa vya nyumbani alivyozawadia wananchi katika hafla hiyo.

Sunday, August 17, 2014

ZITO ANUSURIKAU KUUAWA KISA SUNGURA, ALIPIGWA MTAMA

Mwanafunzi wa Tanzania Aibuka mshindi wa Kwanza Tuzo ya Isha SADC


Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza mwanafunzi wa kidato cha nne Neema Steven Mtwanga(16) anayesoma katika shule ya sekondari Naboti Makambako,Njombe baada ya kuibuka mshindi wa kwanza katika utunzi wa insha katika shindano lililoandaliwa na Jumuiya ya uchumi ya maendeleo kusini mwa Afrika(SADC).Rais Kikwete alimpongeza mwanafunzi huyo wakati wa hafla ya ufunguzi wa mkutano wa 34 wa wakuu wa nchi za SADC unaofanyika katika mji wa kitalii wa Victoria Falls, nchini Zimbabwe ambapo mwanafunzi huyo aliandika insha inayohusu mabadiliko ya tabia nchi.

WAZEE WA DAR ES SALAAM WAWATAKA UKAWA KURUDI BUNGENI

WAZEE 02Mzee Alhaji Sheikh Bakari Chiwaka (kulia) akisisitiza umuhimu wa maridhiano katika mchakato wa Katiba Mpya na kuwa Katiba bora itapatikana kwa uongozi bora na wa kidemokrasia nchini. Kushoto ni Kepteni Mstaafu Alhaji Mohamed Ligora.

RAIS KIKWETE AHUDHURIA MKUTANO WA 34 WA SADC VICTORIA FALLS



Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipokea maua kutoka kwa watoto jana muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa mji wa Victoria Falls nchini Zimbabwe ambapo alishiriki katika mkutano wa 34 wa siku mbili wa wakuu wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika SADC.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Rais Hifikepunye Pohamba wa Namibia muda mfupi kabla ya kuanza kwa mkutano wa 34 wa wakuu wa nchi za SADC unaofanyika katika mji wa Victoria Falls nchini Zimbabwe.

MAZINGIRA YA MTO SIMIYU YANAVYONUFAISHA WAKAZI WAKE


 

MTOTO WA MACHO AFARIKI DUNIA


Mtoto Godwin Florence Rweyemamu (3) enzi za uhai wake akiwa na bibi yake, Elda Charles Rweyemamu.
Na Makongoro Oging'

MTOTO Godwin Florence Rweyemamu (3), mkazi wa Kijiji cha Kamala, Kata ya Bangwe mkoani Kigoma aliyeletwa katika Hospitali ya Taifa jijini Dar es Salaam kwa matibabu ya kansa ya macho amefariki dunia leo asubuhi.
Mtoto Godwin amefariki baada ya kusumbuliwa na kansa ya macho iliyoambatana na malaria na upungufu wa damu mwilini.

WAYNE ROONEY AKARIBIA KUFIKIA MAFANIKIO YA KUJENGEWA SANAMU, AMEDAI BEKI WA ZAMANI WA MAN UNITED PHIL NEVILLE

Statue: Phil Neville says that Wayne Rooney could achieve statue status if his form continues
Sanamu: Phil Neville amsema Wayne Rooney anaweza kufanikiwa kujengewa sanamu kama ataendelea kufanya makubwa.

PHIL Neville amedai kuwa Wayne Rooney anaweza kuwa gwiji wa Manchester United na hata kupata heshima ya kujengewa sanamu katika klabu hiyo.
Beki huyo wa zamani wa United aliyasema hayo wakati anazungumzia nahodha mpya wa klabu na alidai kama mchezaji huyo wa zamani wa Everton anataka,  anaweza kuingia katika orodha ya wachezaji wakubwa zaidi waliowahi kutokea katika historia ya klabu. 

MANCHESTER CITY WAANZA LIGI KUU ENGLAND VIZURI KWA KUIFUMUA 2-0 NEWCASTLE UNITED


Mnyumbulikaji wa Kihispania: David Silva akifunga bao la kuongoza

MABINGWA watetezi wa ligi kuu soka nchini England, Manchester City wameanza vyema kampeni za kutetea taji lao baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 ugenini dhidi ya Newcastle United katika dimba la St. James Park.
Bao la kwanza la Man City katika mechi hiyo iliyomalizika dakika chache zilizopita limefungwa na kiungo mshambuliaji, raia wa Hispania, David Silva katika dakika ya 39' akimalizia vizuri pasi ya Edin Dzeko.