Sunday, August 17, 2014

WAYNE ROONEY AKARIBIA KUFIKIA MAFANIKIO YA KUJENGEWA SANAMU, AMEDAI BEKI WA ZAMANI WA MAN UNITED PHIL NEVILLE

Statue: Phil Neville says that Wayne Rooney could achieve statue status if his form continues
Sanamu: Phil Neville amsema Wayne Rooney anaweza kufanikiwa kujengewa sanamu kama ataendelea kufanya makubwa.

PHIL Neville amedai kuwa Wayne Rooney anaweza kuwa gwiji wa Manchester United na hata kupata heshima ya kujengewa sanamu katika klabu hiyo.
Beki huyo wa zamani wa United aliyasema hayo wakati anazungumzia nahodha mpya wa klabu na alidai kama mchezaji huyo wa zamani wa Everton anataka,  anaweza kuingia katika orodha ya wachezaji wakubwa zaidi waliowahi kutokea katika historia ya klabu. 
"Kama unavunja rekodi ya  Bobby Charlton katika klabu ya Manchester United, unazungumzia heshima ya sanamu," Neville aliwaambia The Mirror.
"Kwasababu amekuwa mchezaji mkubwa kwa wakati wote. Watu wanampenda Wayne Rooney, ninaposema anastahili sanamu, namaanisha kuwa ni mchezaji mkubwa.
Success: Wayne Rooney has won five Premier League titles since joining Manchester United
Mafanikio: Wayne Rooney ameshinda makombe matano ya ligi kuu tangu alipojiunga na Manchester United

No comments:

Post a Comment