Monday, December 19, 2016

PROF: MBALAWA ATOA ONYO KWA UHARIBIFU WA MIUNDO MBINU

 Ujenzi wa barabara ya Mela-Bonga yenye urefu wa KM 88.8 inayojengwa kwa kiwango cha lami ukiendelea. Mradi huo unajengwa na Mkandarasi wa Kampuni ya M/s China Railway Seventh Group na unatajiwa kukamilika mwezi Agosti mwakani.
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akishindilia nondo kwenye moja ya ujenzi wa barabara ya Mela-Bonga yenye urefu wa KM 88.8, inayojengwa kwa kiwango cha lami, alipokuwa akikagua mradi huo.

MKURUGENZI MTENDAJI WA JAMII FORUM HATIMAE KAPEWA THAMANA.

Mwanzilishi wa mtandao wa JamiiForums  Maxence Melo   ameachiwa kwa dhamana leo  katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, baada ya kukaa mahabusu kwa takribani siku 5.a

Melo anakabiliwa na mashtaka matatu likiwemo la kumiliki na kuendesha tovuti ambayo haijasajiliwa hapa nchini Tanzania (JamiiForums).

BAADHI YA MANENO YA KIINGEREZA, KWA KISWAHILI

1. Password - Nywila.
2. Juice - Sharubati.
3. Chips - Vibanzi.
4. PHD - Uzamili
5. Masters - Uzamili
6. Degree - Shahada.
7. Diploma - Stashahada.
8. Certificate - Astashahada.
9. Keyboard - Kicharazio.
10. Scanner - Mdaki.

ATHARI ZA UCHAFUZI WA MAZINGIRA, JIJINI ARUSHA

 

Ngombe na mbuzi wakiwa wamesongamana chini ya mti pekee uliokuwepo  katika eneo lililopo  karibu na Shule ya sekondari ya Oljoro  mkoani Arusha wakifuata kivuli ili kujikinga na jua Desemba 17, 2016.  Uharibifu wa mazingira unaosabishwa na  shughuli za binadamu  hasa ukataji miti hovyo unaathiri hata viumbe wengine kama picha inavyoonyesha.

WAZIRI MKUU, KASSIM MAJALIWA AUNDA KAMATI KUCHUNGUZA KIFO CHA JOHN, ''TEMBO''

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika kikao cha 
 majumuisho ya ziara yake ya mkoa wa Arusha kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Arusha, Desemaba 18, 2016. Kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali imeunda tume kuchunguza taarifa inayoelezea utaratibu uliotumika kumhamisha faru John kutoka Hifadhi ya Ngorongoro kwenda Sasakwa Black Rhino Sanctuary iliyoko kwenye Hifadhi ya Grumeti Serengeti pamoja na kutafuta kaburi la faru huyo.
Amesema timu hiyo ya wataalamu tayari imeshafika Sasakwa  VIP Grumet kwa ajili ya kutafuta kaburi na kuchukua vinasaba vya masalia ya faru John na kisha watakwenda kwenye Hifadhi ya Ngorongoro kuchukua vinasaba vya watoto wake  na kuvilinganisha na pembe hiyo ili  kubaini kama kweli pembe aliyopelekewa ni  ya faru John au laa.