Friday, July 18, 2014

Jeshi la ardhini la Israel laingia Gaza



Israel imeanzisha operesheni ya nchi kavu pamoja na mashambulizi ya anga na baharini dhidi ya vuguvugu la kupigania uhuruwa palestina Hamas katika ukanda wa Gaza.
Katika kipindi cha siku kumi zilizopita zaidi ya wapalestina mia mbili wameuwawa katika mashambulizi ya anga yaliyotekelezwa na Israel na Muisraeli mmoja aliuwawa katika mashambulizi ya mizinga ya roketi kutoka Gaza.(MM)
Oparesheni hiyo ya kupeleka majeshi ya ardhini imenza usiku, ni operation kubwa kufanywa katika kipindi cha miezi mitano.
Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema lengo ni kuharibu kabisa miundo mbinu na silaha zinazotumiwa na vuguvugu la Hamas kuishambulia Israel.

Thursday, July 17, 2014

Shule 10 bora 2013 zaporomo

Shule ya Sekondari Kisirimi iliyopo Wilayani Arumeru mkaoni Arusha  
Na Mussa Juma, Mwananchi
Kwa ufupi

Wednesday, July 16, 2014

PALE AMBAPI SIMBA ANAPO WEKA MTU KATI NA NYATI

                                        

BOSI NUSU AUWAWE KWA RISASI.


INASIKITISHA! Watu wasiojulikana wamemshambulia kwa risasi na mapanga Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu, Geita, Juma Kimisha na msafara wake na kusababisha kiongozi huyo kukimbizwa Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Mwanza ili kuokoa uhai wake.

RAIS KIKWETE AANDAA FUTARI KWA VIONGOZI WA DINI YA KIISLAMU IKULU, DAR ES SALAAM

Kadhi Mkuu wa Tanzania Sheikh Abdullah Yusuf bin Ali bin Yusuf ash-Shirazi Mnyasi (mwenye kipaaza sauti) akiongoza dua katika futari aliyoandaa Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwa viongozi wa madhehebu mbalimbali wa dini ya Kiislamu Ikulu jijini Dar es salaam jioni ya Julai 16, 2014

MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, YATANGANZWA, ZAIDI YA ASILIMIA 85YA WATAHINIWA WAFAULU

top_logo_61f53.gif
Matokeo ya mtihani wa kidato cha 6 yaliyofanyika tarehe Mei 5 – 21, yametoka.
Jumla ya watahiniwa 38,905 sawa na asilimia 95.98 ya watahiniwa waliofanya mtihani kidato cha sita wamefaulu.
Wasichana waliofaulu ni 12,080 na wavulana waliofaulu ni 26,825
Watahiniwa waliopata division IV ni 4,420 sawa na asilimia 12.54
Watahiniwa waliopata zero (0) ni 612 sawa na asilimia 1.74.

UKIMWI KUTHIBITIWA MWAKA 2030

Kuna uwezekano kuwa UKIMWI unaweza kudhibitiwa ifikapo mwaka 2030, kwa mujibu wa taarifa ya shirika la Umoja wa Mataifa.
Shirika hilo- UNAids- limesema idadi ya maambukizi mapya ya virusi vya HIV na vifo vinavyotokana na UKIMWI inapungua.
Hata hivyo, imetoa wito kwa juhudi zaidi za kimataifa kwa kuwa "kasi ya sasa haiwezi kumaliza ugonjwa huo".
Shirika la Madaktari wasio na Mipaka limeonya kuwa wengi wa watu wanaohitaji dawa za kufubaza virusi vya HIV, bado hawawezi kuzipata dawa hizo.

WAFUASI WA CHADEMA NA CCM, NUSRA WAZICHAPE.


 Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, Idd Azzan wa CCM (KULIA), akiamulia ugomvi wa Diwani wa Kimara, Pascal Manota wa Chadema (kushoto) na Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge waliotaka kuzichapa ulipotokea mzozo katika mkutano wa hadhara wa Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla katika Uwanja wa Shule ya Mavurunza, Kata ya Salanga, Jimbo la Ubungo, Dar es Salaam jana.