Shule ya Sekondari Kisirimi iliyopo Wilayani Arumeru mkaoni Arusha
Na Mussa Juma, Mwananchi
Kwa ufupi
Kismiri (pichani) imeshika nafasi ya tatu kati ya
shule 10 bora nchini mwaka huu, kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa
jana na Baraza la Mitihani Tanzania (Necta).
Arumeru. Mwalimu mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kisirimi
wilayani Arumeru, Arusha, Emmanuel Kisongo amesema kufanya vizuri kwa
shule yake ni kuthibitisha shule za kata zinaweza kuwa bora nchini.
Kismiri (pichani) imeshika nafasi ya tatu kati ya
shule 10 bora nchini mwaka huu, kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa
jana na Baraza la Mitihani Tanzania (Necta).
Akizungumza na Mwananchi jana, Mwalimu Kisongo
alisema mwaka huu wanafunzi wa shule yake wamefanya mtihani wa kidato
cha sita kwa mara ya saba na shule imefanikiwa kushika nafasi ya tatu
kitaifa kwa mara ya kwanza.
“Nimefurahi tumeingia kwenye shule 10 bora nchini
mara tano na safari hii tumeshika nafasi ya tatu. Ni wazi shule za kata
zinaweza, tofauti na fikra za wengi kuwa shule zipo chini kielimu,”
alisema.
Kisongo alisema mwaka jana walishika nafasi ya tano, kitaifa na mwaka juzi, walishika nafasi ya tatu kama mwaka huu.
“Siri ya mafanikio yetu ni ufundishaji mzuri na
ushirikiano mzuri wa walimu, wanafunzi na wazazi kwa lengo kubwa la
kuthibitisha kuwa walioanzisha shule ya kata hawakufanya makosa,”
alisema.
Alisema shule yake, ambayo ina jumla ya walimu 32
kati yao 12 wanafundisha kidato cha tano na sita, inafuata michepuo ya
sayansi na sanaa (art) na mwaka huu wanafunzi 52 walifanya mtihani.
“Tunajivunia mafanikio haya na malengo yetu
kuifanya shule hii kuwa bora nchini kwani ipo katika mazingira tulivu na
wanafunzi wa dini zote tunawajenga kuwa na hofu ya Mungu,” alisema.
Alisema kwa sasa wanafunzi wa shule hiyo,
wanajitambua na wanaheshimu masomo yao. Hawana muda wa migogoro na
shule, jambo ambalo linawapa muda mzuri kusoma.
Shule 10 bora 2013 zaporomoka
Ibrahim Yamola, Mwananchi
Dar es Salaam. Shule za sekondari zilizokuwa
kwenye orodha ya Kumi Bora ya matokeo ya kidato cha sita mwaka jana
zimeporomoka, huku shule isiyo maarufu ya Igowole, mkoa wa Iringa
ikichomoza kutoka nafasi ya nane hadi ya kwanza mwaka huu
No comments:
Post a Comment