Saturday, August 16, 2014

TANZANIA MWENYEJI WA MASHINDANO YA MAJESHI YA AFRIKA MASHARIKI


 0114
Mkuu wa Bregedi ya Nyuki ambae ni Makamo Mwenyekiti wa michezo ya Majeshi Bregedia Jenerali Sharif Sheikh Othman akizungumza na waandishi wa habari kuhusu michezo ya nane ya Majeshi ya Jumuia ya Afrika Mashariki. Mkuta huo umefanyika huko Bregedi ya Nyuki Migombani Zanzibar.

MAN UNITED, YAANZA VIBAYA LIGI KUU BAADA YA KUFUNGWA 2-1 NA SWANSIA CITY

Friday, August 15, 2014

Sitta: Hatuwezi kusitisha mikutano Bunge la Katiba


Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta akizungumza na wafugaji kutoka mikoa mbalimbali nchini walipomtembelea ofisini kwake Dodoma jana. Wafugaji hao walipelekwa bungeni hapo na Mjumbe wa Bunge hilo ambaye pia ni Mbunge wa Maswa Magharibi, John Shibuda (kushoto). Picha na Emmanuel Herman
Mwenyekiti wa Bunge la Katiba, Samuel Sitta amesema mikutano ya Bunge hilo haiwezi kusitishwa na kwamba itaendelea kwa kuwa idadi ya wajumbe waliopo inakidhi matakwa ya kisheria kutunga Katiba.
Kadhalika Sitta amewatuhumu wajumbe wa wanatokana na kundi la Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kwamba si wazalendo kutokana na kususia Bunge hilo tangu Aprili 25, mwaka huu.(Imakulata Ng'elenge)

Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na Uchumi Supermarkets Tanzania Limited (USL) zatiliana saini kukuza biashara

1(16)
Mkurugenzi wa Uendelezaji Biashara wa NHC, David Shambwe akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini hati ya makubaliano kati ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na Uchumi Supermarkets Tanzania Limited (USL), leo mchana, makubaliano hayo yataziwezesha pande hizo mbili kushirikiana kibiashara ambapo USL itapewa kipaumbele kwenye kupanga katika miradi ya ujenzi ya majengo ya Shirika la Nyumba la Taifa popote nchini.
2
Meneja Mkuu wa Uchumi Supermarkets Tanzania, Chriss Lenana akifafanua Jambo kwenye tukio hilo la utiani saini makubaliano baina ya pande hizo mbili, lililofanyika kwenye hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam leo.

Serikali yasema hakuna Ebola Tanzania


erikali ya Tanzania yathibitisha kutokuwepo kwa ugonjwa huo
Tanzania imesema haina mgonjwa aliyethibitishwa kuwa na ugonjwa wa Ebola.
Kauli hiyo inakuja baada ya kufanyiwa uchunguzi kwa wagonjwa wawili waliotiliwa shaka kuwa na ugonjwa huo.
Waziri wa Afya wa Tanzania Seif Rashid ameiambia BBC, wagonjwa hao waliohisiwa kupata maambukizo kutokana na dalili za awali, ni wa kutoka Benin na Mtanzania, lakini vipimo vimeonesha hawana maambukizo hayo.

Thursday, August 14, 2014

WANANCHI WAFANYA MAANDAMANO NA KUUA MBWA WALIOMUUA MWANAFUNZI NA KUMLA NYAMA.

 ???????????????????????????????
???????????????????????????????
Mbwa waliomuua mwanafunzi  Ibrahimu Chipungahelo wakiwa wameuwawa na wananchi wenye hasira kali.

OFISI YA CHADEMA KATA YA RUAHA JIMBO LA IRINGA MJINI YACHUKULIWA NA CCM BAADA YA CHADEMA KUSHINDWA KULIPA KODI

IMG_9966Katibu wa CCM kata ya Ruaha Rashid Shungu ( wa  pili  kushoto ) na kada wa Chadema aliyehamia CCM Ibrahim Mmasi  pamoja na  wanachama  wengine wa CCM wakiwa  wameshika bendera ya CCM ambayo itapepea katika ofisi mpya ya kata ya Ruaha ,ofisi ambayo awali ilikuwa ikimilikiwa na Chadema kabla ya  kufukuzwa kwa  kushindwa kulipa deni la kodi kiasi cha Tsh 540,000 , kushoto fundi rangi akiendelea  kupaka rangi ya CCM

RAIS KIKWETE AFUNGUA MKUTANO WA KWANZA WA DIASPORA JIJINI DAR ES SALAAM LEO

II with No comments
di1
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifungua mkutano wa kwanza wa Diaspora katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam leo Agosti 14, 2014

Ukawa waombwa kurudi Bungeni


UKAWA waombwa kukubali maoni ya watanzania walio wengi ya kuheshimu pesa za walipa kodi kwa kurudi bungeni na kupingana kwa hoja kwani hoja zao zikiwa za huakika hazitapingwa bali kanuni na taratibu zinazoendesha bunge zitafuatwa badala ya kuendelea kulalamika katika majukwaa ya kisiasa.

Kauli hiyo imetolewa na balozi wa amani Tanzania Risasi Mwaulanga alipokuwa akiongea na waandishi wa habari katika ukumbi wa habari maelezo leo jijijni Dar es Salaam.

WAKAZI WA KIMARA JIJINI DAR ES SALAAM WATISHIA MAISHA YAO ILI KUCHOTA MAFUTA ,BAADA YA LORI KUPINDUKA


Lori la mafuta baada ya kuanguka.
Polisi wakipakia madumu ya mafuta waliyoyakamata kutoka kwa wananchi.…

NMB YAZINDUA TAWI LA NANYUMBU.


NMB katika kuongeza idadi ya matawi yake na kuhakikisha inawafikia watanzania wengi na kila kona nchini, jana imezindua tawi jipya la wilaya mpya ya Nanyumbu katika mkoa wa Mtwara.
Kwa sasa NMB imefikisha matawi Zaidi ya 150 na wateja Zaidi ya milioni 2 huku ikijivunia ATM mashine Zaidi ya 500 nchi nzima. Hiyo ni idadi kubwa kuliko benki yoyote Tanzania.

KIJANA COLINS SILVANUS, AKANA KUA HANA UGOMVI NA MLEZI WAKE

Mtoto Colins Silvanus Mzeru mkazi wa Tabata Dar es Salaam, akizungumza na waandishi wa habari Dar es salaam jana alipofika na mamayake mlezi, Nora Mzeru kukanusha tuhuma dhid i ya mamayake huyo kuwa amemfungia na kumtesa kwa muda mrefu sasa na kushindwa kwenda shule.

Colins amesema mama yake huyo mlezi hana tatizo nae na amekuwa akiishi nae kwa muda mrefu sasa vizuri tangu kufariki kwa mama yake mzazi na yeye kuchukuliwa na baba yake na kupokelewa bna mama yake huyo aliyekuwa akiishi na baba yake na kulelewa vizuri hadi sasa licha ya kuwa baba yake mzazi nae kufariki.

Wednesday, August 13, 2014

PHIRI AJARAJIWA KUFIKA SIMBA LEO.

Kocha mpya wa Simba, Mzambia Patrick Phiri

Kocha mpya wa Simba, Mzambia Patrick Phiri, anatarajia kuwasili nchini leo kwa ajili ya kusaini mkataba wa kuanza kukinoa kikosi cha timu hiyo kinachojiandaa na msimu ujao wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara itakayoanza Septemba 20, mwaka huu.

Phiri anakuja nchini kuchukua mikoba ya Mcroatia Zdravko Logarusic ambaye Jumapili wiki hii alitimuliwa na uongozi wa klabu hiyo ya Mtaa wa Msimbazi, Kariakoo jijini Dar es Salaam.

Sunday, August 10, 2014

UJENZI BARABARA YA MBEYA CHUNYA UNAKWENDA KASI



Kipande cha barabara cha lami kutoka Lwanjilo hadi Chunya Mjini 

WAPO WALIOFUNGA NA WAPO WALIOSHINDA NJAA MWEZI WA RAMADHANI...

Na Mathias Canal, Kwanza Jamii-Iringa
Kufunga kunahitaji kujitoa hakika ili kupata thawabu kwa mwenyezi mungu lakini wapo waliofunga kwa shinikizo la wenza, dini, rafiki, ndugu na hata jamaa zao wa karibu.
Lengo la kufunga wakati mwingine ni kuondoa na kuzuia tama zote unazokuwa nazo
1. kufunga ni Amri: (umma wa nabii Musa na Issa, wao walikua wanafunga kila mwezi siku tatu na siku ya Ashura (inajulikana kama Pass ver au Pasakha) lakini wanaofunga sasa walipunguziwa siku.
2. kufunga kunafuta Madhambi (Mizigo). Mungu amesema katika sura#33 aya#35. Ukijaaliwa pata thawabu, itafute uisome, I have run out of space.
Mke wa mtume (s.a.w) Ummu Salama, alimuuliza Mtume "wamaume mnatajwa kwenye Qurani sisi Je? Siku ile ile saa za Adhuhuri aya hii ikashuka.

ARSENAL YA SHINDA 3-0 DHIDI YA MAN CITY NA KUTWAA UBINGWA WA NGAO YA JAMII

Arsenal wakiwa na Ngao ya Jamii baada ya kuipiga Manchester City 3-0.
Santi Carzola akishangilia bao lake la kwanza kwa Arsenal.…

Arsenal sent out a statement of intent for the season as they impressively dismissed Manchester City in the Community Shield at Wembley.

Arsenal lift the Community Shield
10 August 2014 Last updated at 16:23 GMT
Arsenal sent out a statement of intent for the season as they impressively dismissed Manchester City in the Community Shield at Wembley.
The FA Cup winners took the lead through Santi Cazorla's angled shot and added to that when Aaron Ramsey drove in a strike to finish a counter-attack.
Premier League champions City came close when Stevan Jovetic had a header hit the post and a shot saved.
But Olivier Giroud's dipping 25-yard strike secured Arsenal's win.

JK AKUTANA NA RAIS WA KENYA UHURU KENYATTA.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Rais Uhuru Kenyatta walipokutana katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dubai waliposimama kwa muda wakiwa njiani kuelekea nyumbani wakitokea Washington DC, Marekani, walikohudhuria Mkutano wa Marekani na Wakuu wa nchi wa Afrika ulioandaliwa na Rais Barack Obama.

KAMA MNATAKA MALI MTAIPATA SHAMBANI!!

1. Karudi baba mmoja, toka safari ya mbali,
Kavimba yote mapaja, na kutetemeka mwili,
Watoto wake wakaja, ili kumtaka hali,
Wakataka na kauli iwafe maishani.
2. Akatamka mgonjwa, ninaumwa kwelikweli,
Hata kama nikichanjwa, haitoki homa kali,
Roho naona yachinwa, kifo kimenikabili,
Semeni niseme nini, kiwafae maishani.