Thursday, August 14, 2014

WAKAZI WA KIMARA JIJINI DAR ES SALAAM WATISHIA MAISHA YAO ILI KUCHOTA MAFUTA ,BAADA YA LORI KUPINDUKA


Lori la mafuta baada ya kuanguka.
Polisi wakipakia madumu ya mafuta waliyoyakamata kutoka kwa wananchi.…


Lori la mafuta baada ya kuanguka.
Polisi wakipakia madumu ya mafuta waliyoyakamata kutoka kwa wananchi.
Foleni iliyosababishwa na ajali hiyo eneo la Kimara, Dar.
Polisi wakidumisha ulinzi eneo la ajali.
Gari la zimamoto likiwa eneo la tukio.
Gari lililoanguka.
Kazi ya kuhamisha mafuta kutoka kwenye gari lililoanguka kwenda jingine ikifanyika.
Ni madumu mengine ya mafuta yaliyokuwa yameibiwa.
Polisi wakitafuta mafuta yaliyoibiwa katika moja ya maduka ya jirani.
Wananchi wakiwa pembeni baada ya kufyatuliwa mabomu ya machozi.
Na Gabriel Ng’osha/GPL
GARI lenye namba T748 ABJ lililokuwa limebeba mafuta ya diseli kutoka Dar es Salaam kwenda Singida, limeanguka leo asubuhi na kusababisha foleni ndefu maeneo ya Kimara-Darajani jijini Dar es Salaam.
Dereva wa gari hilo aliyefahamika kwa jina moja la Juma, alikimbizwa hospitali.  Gari hilo lilikuwa na lita 34,000 za mafuta, mali ya Nassor Filling Station ya jijini Dar es Salaam.
Hata hivyo wananchi wa maeneo hayo, badala ya kutoa msaada, walianza kuiba mafuta hayo kabla ya kutawanywa na polisi waliofyatua mabomu ya kutoa machozi na juhudi za kulitoa barabarani zikaanza mara moja.
 

No comments:

Post a Comment