Jeshi la Polisi mkoa wa morogoro linawashikilia watu kumi na wawili kwa
tuhuma za kumjeruhi na kumchoma mdomomi mkuki uliotokezea shingoni
Augustino Pius mkazi wa kijiji cha Dodoma Isanga wilayani kilosa ambapo
saba kati yao tayari wamekifishwa mahakamani.
Akiongea na waandishi wa habari kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa
morogoro Ulrich Matei amesema kuwa wafugaji jamii ya kimasai wilayani
kilosa mkoani morogoro waliwashambulia wakulima kwa silaha za jadi na
kuwajeruhi watu sita mara baada ya kukamatwa kwa mifugo ilioyokuwa
inaharibu mazao shambani.
Wakati huo naibu katibu wa chama cha wafugaji Tanzania Joshua Lugaso
amesema kitendo cha mfugaji kumchoma mkuki Augustino Pius kinalaaniwa
vikali na uongozi wa wafugaji na wafugaji wenyewe huku akivitaka vyombo
vya sheria kuchukua hatua dhidi ya wahusika
No comments:
Post a Comment