Sunday, August 17, 2014

MANCHESTER CITY WAANZA LIGI KUU ENGLAND VIZURI KWA KUIFUMUA 2-0 NEWCASTLE UNITED


Mnyumbulikaji wa Kihispania: David Silva akifunga bao la kuongoza

MABINGWA watetezi wa ligi kuu soka nchini England, Manchester City wameanza vyema kampeni za kutetea taji lao baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 ugenini dhidi ya Newcastle United katika dimba la St. James Park.
Bao la kwanza la Man City katika mechi hiyo iliyomalizika dakika chache zilizopita limefungwa na kiungo mshambuliaji, raia wa Hispania, David Silva katika dakika ya 39' akimalizia vizuri pasi ya Edin Dzeko.
Mshambuliaji hatari wa Argentina, Sergio Kun Aguero aliifungia City bao la pili katika dakika za nyongeza.
Huu ni mwanzo mzuri kwa kocha Manuel Pellegrini mwenye kibarua kizito cha kulibakisha kombe Etihad mbele ya makocha wenzake wa kiwango cha dunia akiwemo Louis Van Gaal (Manchester United), Jose Mourinho (Chelsea), Brendan Rodgers (Liverpoool) na Aserne Wenger (Asernal).
Kikosi cha Newcastle: Krul, Janmaat, Williamson, Coloccini, Dummett, Colback, Anita (Obertan 63), Sissoko, Cabella, Gouffran (Aarons 74), Riviere (Perez 84).

Wachezaji wa akiba: Haidara, Elliot, Steven Taylor, Abeid.
Kikosi cha Man City: Hart, Clichy, Demichelis, Kompany, Kolarov, Fernando, Toure, Nasri (Milner 78), Jovetic (Fernandinho 73), Silva, Dzeko (Aguero 83).

Wachezaji wa akiba: Zabaleta, Caballero, Jesus Navas, Boyata.
Kadi za njano: Silva, Demichelis, Kolarov, Kompany.
Mwamuzi: Martin Atkinson (W Yorkshire)

BAADA YA MECHI ZA LEO NA JANA, MSIMAMO WA LIGI KUU ENGLAND UKO HIVI
PosTeamPWDLGFGAGDPts
1Manchester City11002023
2Arsenal11002113
3Liverpool11002113
4Swansea City11002113
5Aston Villa11001013
6Hull City11001013
7Tottenham Hotspur11001013
8Everton10102201
9Leicester City10102201
10Sunderland10102201
11West Bromwich Albion10102201
12Burnley00000000
13Chelsea00000000
14Crystal Palace100112-10
15Manchester United100112-10
16Southampton100112-10
17Queens Park Rangers100101-10
18Stoke City100101-10
19West Ham United100101-10
20Newcastle United

No comments:

Post a Comment