Sunday, June 1, 2014

AMFUNGA MAMA YAKE MZAZI MIAKA 2

“Siwezi kukupa comment (maoni) kwa sababu lipo kwenye uchunguzi maana suala hili nimewapatia polisi walifanyie uchunguzi, kwa hiyo wakishamaliza utaratibu wa kuchunguza wakapata ukweli wa hili jambo watanipa taarifa hivyo nitakuwa kwenye position (nafasi) ya kusema kwa hiyo nategemea kuletewa taarifa kamili kwa maandishi,” anasema Kilasi.
Hata hivyo Evaristo Ng’ande, kijana anayedaiwa kumfungia ndani mama yake huyo wa kambo alipotafutwa kutolea ufafanuzi suala hilo alisema hawezi kuzungumza chochote kwa kuwa ameshatoa maelezo polisi hivyo anasubiri polisi wakamilishe uchunguzi wao wampeleke mahakamani.
“Yaani habari za mgonjwa huyo mimi siwezi kusema chochote maana maelezo yangu nimeshatoa polisi na kesi yangu iko polisi, kwa hiyo nasubiri wakamilishe uchunguzi wao nipelekwe mahakamani,” alisema Ng’ande kwa kifupi.

Hata hivyo baada ya maelezo hayo baadaye kijana huyu alipiga simu kwa mmoja wa waandishi wa gazeti hili, na kumweleza kuwa hajamtelekeza mama huyo bali kinachofanyika ni majungu kutoka kwa baadhi ya majirani zake wasiopenda maendeleo.
“Unajua kaka hapa Igwachanya pana majungu sana ila mama mdogo sijamterekeza na hana mtoto mwingine wa kumtegemea zaidi yangu mimi, ni kweli hili duka ni lake na nyumba yake ila kulingana na mazingira uliyomkuta nayo hawezi kukaa kwa sasa dukani, hata hivyo mimi nimeweka hela zangu nyingi tu maana lilikuwa na mtaji usiozidi milioni mbili na nusu na huwa nampa taarifa za mauzo,” anasema.

No comments:

Post a Comment