Mbunge wa
Viti Maalum CCM Mkoa wa Iringa Ritta Kabati (wa pili kushoto)
akiwatuliza vijana wanaoendesha bajaji mjini Iringa nje ya ofisi za
Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi kavu na Majini (SUMATRA) baada ya
mbunge huyo kuongea na Afisa Mfawidhi wa SUMATRA Mkoa wa Iringa, Rahim
Kondo leo mchana, ambapo vijana hao walidai kusumbuliwa na SUMATRA
wanapofanya kazi zao. Hata hivyo afisa wa sumatra alikanusha madai hayo
na kusema kuwa vijana hao hawataki kufuata taratibu zilizowekwa na
mamlaka hiyo. (PICHA NA FRIDAY SIMBAYA)
Mbunge wa
Viti Maalum CCM Mkoa wa Iringa Ritta Kabati (kushoto) akiongea na
Mwandishi wa Kwanza Jamii na kuelezea mkasa mzima wa malalamiko ya
vijana wa Bodaboda mchana wa leo.
Mwenyekiti wa Bodaboda mjini iringa, Mwambobe akiongea na KwanzaJamii leo katika ofisi za Ikolo Investment Ltd zilizopo jengo la NSSF Akiba House
No comments:
Post a Comment