Mwanafunzi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Tumaini Iringa, Vincent Lugendo (katikati) akifurahia Tv.
Mkazi wa Frelimo A, Mzee Mahmoud Juma Tagalile, 64 akielezea jinsi alivyopata bahati ya kushinda TV kwa MC
Mwanafunzi
wa mwaka wa tatu katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Tumaini- Iringa,
kitivo cha sheria, Vincent Lugendo ameshinda TV katika shindano la
Coca–Cola la Jionee Mwenyewe Kombe la FIFA la Dunia mwaka 2014,
alikuwepo pia Mzee Mahmoud Juma Tagalile, 64 mkazi wa Frelimo A,
Manispaa ya Iringa, imefahamika.
Kampuni
ya vinywaji baridi ya Coca-Cola Kwanza leo imekabidhi zawadi ya luninga
mpya aina ya Sony BRAVIA FIFA WORLD CUP 32, FIFA OFFICIAL TV, kwa
washindi 14 wa shindano la Coca-Cola la Jionee Mwenyewe Kombe la FIFA la
Dunia, mkoani Iringa.
Akikabidhi
zawadi hizo, Afisa Mauzo na Masoko Nyanda za Juu Kusini/kati (Iringa,
Njombe na Ruvuma), Mrisho Ramadhani alitoa rai kwa Watanzania kushiriki
shindano ambalo zawadi yake ya juu ni tiketi za kwenda nchini Brazil
kushuhudia mchezo wa robo fainali wa Kombe la FIFA la Dunia. Zawadi
nyingine ni televisheni, mipira maalumu ya Kombe la Dunia na fulana.
Akabidhi
zawadi kwa washindi 14 wa mkoa wa Iringa katika Stendi Kuu ya mabasi
yaendao mikoni leo mchana, afisa mauzo na masoko huyo aliwaomba wananchi
kushiriki mara kwa mara ili kupanua wigo wa kujishindia zawadi
mbalimbali.
Wakizungumza
baada ya kukabidhiwa zawadi zao, washindi wote walionesha kuzifurahia
na kusema kuwa shindano hilo ni halisi na kwamba kila mtu anaweza
kuibuka mshindi, ambapo kila mmoja wa alikabidhiwa TV inchi 32 yenye
thamani ya shilingi 900,000/- (sawa na shilingi 12,600000/- kwa TV 14).
Washindi
wanapatikana kwa kunywa soda ya chupa ya Coca- Cola na kupata vizibo
viwili vyenye kutengeneza neno Brazil pamoja na kizibo cha ushindi.
Kizibo
cha ushindi kina picha ya kitu ambacho mteja ameshinda (Tv, Mpira au
T-shirt) wakati kizibo cha ushindi wa zawadi ya tiketi kina nembo ya
ndege.
Kampuni
ya Coca-Cola ni mshirika wa Fifa kwa muda mrefu, ambapo uhusiano rasmi
ulianza tangu 1974 na kuwa mdhamini rasmi wa michuano ya Kombe la Dunia
1978. Coca-Cola imekuwa na matangazo kwenye viwanja vinavyochezewa
michuano ya Kombe la Dunia tangu 1950
No comments:
Post a Comment