Saturday, April 26, 2014

BBQ NYAMA CHOMA (HOME)

Nyama ya mbuzi mbavu na inawekewa marination ya kawaida tu ili kuilainisha na kuipa ladha kabla ya kuichoma. Tunatumia tangawizi,kitunguu saumu,ndimu au limao na chumvi.Nyama inapakwa hivyo vyote kisha inawekwa kwenye fridge kama lisaa hivi ndio inaanza kuchomwa.Inaweza kuwekwa hivyo vyote hata usiku ikalala kwenye fridge kesho yake ikachomwa.
Kuku nao huwekwa marination ila hii ni kitunguu saumu na limao na chumvi.Wakati mwingine tunaweza kufanya chicken tandoor kama tunataka ile ladha ya pilipili.
Hii ni mbuzi ikiiva taratibu….
 Mambo yako tayari kuliwa..
LUNCH:Mbuzi choma,ugali,kachumbari na mboga ya majani ya maboga.
DINNER:Kuku choma,ndizi tamu za kukaaanga na kachumbari bila kusahau chachandu.

Jumapili ikawa imeishia hapo.Kama ipo ndani ya uwezo wako unaweza kujibajeti vizuri ukafanya nyumbani. Sio kwamba unanunua mbuzi mzima mbuzi kilo mbili hata moja inatosha kulingana na ukubwa wa familia yako.Kuku mmoja,wawili au watatu pia wanatosha.Sio mpaka tukale kuku au mbuzi bar hata nyumbani vinawezekana tu hasa baba akiwa ndio kashika usukani

No comments:

Post a Comment