Saturday, May 17, 2014

NAHITAJI MILIONI 700,000 KUOKOA MAISHA YANGU.

Ugonjwa wa saratani unazidi kushika kasi kila kukicha hapa nchini. Pia umegharimu maisha ya watu wengi kutokana na huo ugonjwa bado haujapatiwa tiba madhubuti.
Mbali na kugharimu maisha ya watu wengi, ugonjwa huu umekuwa tishio kutokana na gharama kubwa za matibabu zinazowagharimu wagonjwa.

Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa Februari wakati wa maadhimisho ya Siku ya Saratani Dunia, takwimu zinaonyesha kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara, zenye ongezeko kubwa la wagonjwa wa saratani.(Martha Magessa)
Takwimu hizo zinaeleza kuwa kila mwaka wagonjwa wapya 21,180 hugundulika. Aidha zaidi ya watu 16,000 hufariki dunia kila mwaka kutokana na ugonjwa huo. Kati ya wagonjwa 40,000 wanaokwenda kutibiwa kwenye hospitali maalumu, asilimia 80 ya wagonjwa hao wanafariki dunia kutokana na maradhi ya saratani.
Licha ya ugonjwa huo kugharimu maisha ya watu wengi, baadhi ya wagonjwa wanaogundulika mapema, wataalamu wa afya huwashauri wafayiwe upasuaji kwa lengo la kuondoa sehemu iliyoathirika na kuzuia usienee sehemu zingine za mwili na kuleta madhara zaidi.
Hali hiyo imemkuta kijana Gerard Mwambungu mkazi wa Manzese jijini Dar es Salaam, ambaye ameamua kupiga magoti mbele ya Watanzania akiwaomba msaada wa fedha ili aweze kupata matibabu na kunusuru maisha yake.
Mwambungu ambaye hakuwahi kutegemea kama siku moja angekumbwa na maradhi hayo, sasa nusura ya maisha yake iko mikononi kwa Watanzania.
Kijana huyo amekuwa akisumbuliwa na saratani ya ngozi kwa muda wa takriban miezi saba. Licha ya kwamba baada ya kuanza kuumwa hakufahamu kuwa ingefika hatua ya kufanyiwa upasuaji.
Mwambungu aliyekuwa mfanyabiashara wa viatu katika eneo la Kituo Kikuu cha Mabasi ya Mikoani cha Ubungo, baada ya kufanyiwa vipimo na wataalamu wa afya katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kugundulika na ugonjwa huo kwenye mguu wake wa kulia sasa anatakiwa kufanyiwa upasuaji.
Chimbuko la ugonjwa huo
Mwambungu anasema siku moja jioni baada ya mizunguko yake ya kutafuta riziki alikuwa amejipumzisha sebuleni kwake. Akiwa hana hili wala lile, akajisikia muwasho sehemu ya mguuni. Anasema kwanza aliinama na kuangalia ule muwasho kama ni mkwaruzo alioupata akiwa kwenye mizunguko ya siku ile au la.
Hata hivyo Mwambungu anasema haukuwa mkwaruzo kama alivyodhania bali kilikuwa ni kipele, kitu ambacho hakikumtia hofu, kwani haikuwa mara ya kwanza kutokewa na kipele mwilini mwake, basi akajikuna usiku ukapita.
CHANZO:MWANANCH

No comments:

Post a Comment